d Kut 32:8; 34:17; Law 19:4; 26:1; Kum 4:15-23; 27:15; 2Sam 7:22; 1Fal 14:9; 2Fal 17:12; Isa 42:8; 44:9
Exodus 20:1-6
Amri Kumi
(Kumbukumbu 5:1-21)
1 aNdipo Mungu akasema maneno haya yote: 2 b“Mimi ndimi Bwana Mwenyezi Mungu wako, niliyekutoa Misri, kutoka nchi ya utumwa.3 cUsiwe na miungu mingine ila mimi.
4 dUsijitengenezee sanamu katika umbo la kitu chochote kilicho juu mbinguni, au duniani chini, au ndani ya maji. 5 eUsivisujudie wala kuviabudu; kwa kuwa Mimi, Bwana Mwenyezi Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu, ninayewaadhibu watoto kwa ajili ya dhambi za baba zao hadi kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao, 6 flakini ninaonyesha upendo kwa maelfu ya vizazi vya wale wanipendao na kuzishika amri zangu.
Copyright information for
SwhKC