Exodus 20:1-6

Amri Kumi

(Kumbukumbu 5:1-21)

1 aNdipo Mungu akasema maneno haya yote:

2 b“Mimi ndimi Bwana Mwenyezi Mungu wako, niliyekutoa Misri, kutoka nchi ya utumwa.
3 cUsiwe na miungu mingine ila mimi.
4 dUsijitengenezee sanamu katika umbo la kitu chochote kilicho juu mbinguni, au duniani chini, au ndani ya maji. 5 eUsivisujudie wala kuviabudu; kwa kuwa Mimi, Bwana Mwenyezi Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu, ninayewaadhibu watoto kwa ajili ya dhambi za baba zao hadi kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao, 6 flakini ninaonyesha upendo kwa maelfu ya vizazi vya wale wanipendao na kuzishika amri zangu.
Copyright information for SwhKC